Mapato bandarini yaongezeka zaidi

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kupungua kwa mizigo bandarini
kumeathiri si Tanzania pekee bali dunia nzima na kwamba kubanwa kwa mianya
ya wizi kumesababisha kuongezeka kwa mapato kutoka Sh bil 458 Aprili mwaka
huu kufikia Sh bil 517.
Aidha, TRA imesema itaanza uhakiki wa namba za utambulisho wa mlipakodi
(TIN) kutokana na kuwepo watu wenye namba mbili na wasiohakiki watalazimika
kudaiwa kodi na TRA.
Akizungumza katika mkutano na wanahabari jana, Kamishna wa TRA, Alphayo
Kidata alisema upungufu huo wa mizigo bandarini umezikumba pia bandari za
Beira, Msumbiji, Mombasa, ... more »
No comments:
Post a Comment